Mamlaka ya mawasiliano nchini (TCRA)
imetoa onyo pamoja na kuutaka uongozi wa Clouds TV kuomba radhi
Watanzania kupitia taarifa zake za habari ndani ya siku tano mfululizo
kuanzia leo.
Adhabu hiyo imetolewa leo na kamati ya
Maudhui ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), baada ya baadhi ya
wananchi hususani watazamaji wa kipindi cha ‘Take One’ kilichorushwa 28
Juni mwaka huu ambacho kilidaiwa kurusha hewani kipindi hicho
kilichozungumzia masuala ya mapenzi ya jinsia moja (Ushoga) na hivyo
kulalamikiwa na wananchi kwamba kwamba kilikiuka maadili ya taifa kwani
kipindi hicho kiliwakwaza pamoja na kuwasababishia usumbufu
wananchi hususani watazamaji kwa kuwasilisha mada inayozungumzia masuala
ya mapenzi ya jinsia moja (ushoga).
Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo, Bw.
Joseph Mapunda amesema kuwa maamuzi hayo yamefikiwa baada ya wajumbe wa
kamati kutafakari maelezo ya utetezi yaliyotolewa na uongozi wa Clouds
TV.
Post a Comment