Ripoti iliyotolewa na
shirika la kuhudumia watu wanaoishi na virusi vya UKIMWI nchini
Tanzania, TACAIDS inaeleza kuwa hadi kufikia mwaka 2015 takribani
watanzania milioni 1.4 walikuwa wakiishi na virusi vya ukimwi. Idadi hii
imeelezwa kuwa ni sawa na asilimia saba (7%) ya watu wote wamaoishi na
virusi vya UKIMWI, Mashariki na Kusini mwa Afrika.
Kati ya watu hao milioni
1.4 wanaoishi na virusi hivyo, inakadiriwa kuwa watu laki nane
(800,000) walikuwa wakitumia dawa za kupunguza makali ya virusi vya
UKIMWI (ARVs) hadi kufikia nusu ya kwanza ya mwaka 2016. Hii ni sawa na
asilimia 53 ya watu wote wanaoishi na virusi hivyo.
Kuhusu kasi ya
maambukizi ya virusi hivyo, takwimu kutoka UNAIDS zinaonyesha kuwa kuwa
katika kipindi cha mwaka 2015, takribani watu elfu 54 walipata na
maamukizi mapya.
Kufuatia hali hiyo,
jitihada mbalimbali ambazo zimefanywa zinaonyesha kuzaa matunda katika
kupunguza kasi ya maambukizi mapya ambapo kati ya mwaka 2010 hadi 2015,
kasi ya maambukizi mapya imepungua kwa asilimia 20.
ILI KUSOMA HABARI ZA UHAKIKA KILA SIKU DOWNLOAD APP YETU YA ZOTE KALI BLOG KWENYE SIMU YAKO BONYEZA
HAPA
NI BUREE
Post a Comment