Winga
Shiza Ramadhani Kichuya amemaliza ukame wa kutofumania nyavu na
kuchagiza ushindi wa Simba wa magoli 2-1 dhidi ya Yanga katika mchezo wa
ligi Kuu ya Tanzania bara.
Kichuya
sasa anaonekana kuwa na kismati na Yanga, kwani katika mchezo uliopita
aliisawazishia Simba goli kwa mkwaju mzuri wa mpira wa kona uliojaa
wavuni.
Lakini
jana tena aliifanya Simba ifikishe pointi 54 na kuongoza ligi, kwa
kutengeneza goli la kusawazisha na kisha baadaye akafunga goli bora
kabisa la shuti la mbali.