Hatua hiyo imekuja mara baada ya timu hiyo msimu huu kutofanya vizuri na kupoteza nafasi ya kushiriki michuano ya kimataifa baada ya kukosa nafasi kwenye Ligi Kuu na Kombe la FA.
Mwenyekiti wa timu hiyo, Nassor Idrissa ‘Father’, ameliambia BINGWA kwamba kitendo cha kupoteza nafasi hizo bodi ya wakurugezi ya Azam imeamua kumwachia majukumu kocha huyo ili kuhakikisha msimu ujao hayajirudii makosa tena.
“Suala la usajili kwa sasa hatutaki kukurupuka, tunasubiri ripoti ya mwisho kutoka kwa Cioaba na kuangalia nani anakatwa na wanaondelea, hili jambo litafanyika mapema kabla ya kocha huyo kwenda mapumziko,” alisema.
Post a Comment