Kipa wa zamani wa Mtibwa Sugar, Shaaban Kado amerejea kwa mara nyingine katika kikosi hicho kwa kujifunga miaka miwili ya kuitumikia klabu hiyo katika msimu ujao ujao wa 2017/18.
Kado aliwahi kuidakia Mtibwa Sugar katika miaka ya nyuma kabla ya kutimkia Yanga na baadaye kurudi katika timu hiyo kuelekea Mwadui FC aliyoichezea msimu uliopita.
Kocha Mkuu wa Mtibwa Sugar, Shabani Katwila alisema tayari wamemsainisha kipa huyo kwa ajili ya kuitumikia Mtibwa Sugar kwa ajili ya msimu ujao.
Post a Comment