banner

July 26, 2017

USAJILI SIMBA, YANGA NI UTATA, KUMBE MAJINA YA OKWI, AJIBU HAYATAMBULIKI TFF

USAJILI SIMBA, YANGA NI UTATA, KUMBE MAJINA YA OKWI, AJIBU HAYATAMBULIKI TFF

Shirikisho la Soka la Tanzania (TFF) limezikumbusha klabu zote ambazo zinasimamiwa na shirikisho hilo kuhakikisha zinamaliza zoezi lake la usajili mapema.
TFF imetoa tamko hilo kupitia kwa Ofisa Habari, Alfred Lucas kuwa katika timu 16 za Ligi Kuu ya Tanzania Bara ni mbili pekee ndizo ambazo zimewasilisha majina yao ya usajili kuelekea msimu ujao wa 2017/18.

Katika majina ya klabu hizo, Simba na Yanga siyo miongoni mwao, hiyo inamaana kuwa kumbe hata wachezaji wao wapya waliosajiliwa hivi karibuni bado hawatambuliki ndani ya mfumo wa usajili wa shirikisho hilo.
Baadhi ya wachezaji waliosajiliwa hivi karibuni ni Emmanuel Okwi kwa upande wa Simba na Ibrahim Ajibu upande wa Yanga.
Alfred amesema timu 24 za Ligi Daraja la Kwanza na 24 Ligi Daraja la Pili zinatakiwa kukamilisha mfumo wa usajili kwa kuwa imesalia wiki moja tu kabla ya mfumo kufungwa.
Dirisha la usajili lilifunguliwa Juni 15, mwaka huu na litarajia kufungwa Agosti 6, mwaka huu.

Post a Comment

Whatsapp Button works on Mobile Device only

Start typing and press Enter to search