banner

August 27, 2018

KIONGOZI MKUBWA NDANI YA STAND UNITED NA TFF AFUNGIWA MAISHA KUJIHUSISHA NA SOKA

KIONGOZI MKUBWA NDANI YA STAND UNITED NA TFF AFUNGIWA MAISHA KUJIHUSISHA NA SOKA

Kamati ya maadili ya Shirikishla Soka Tanzania (TFF) imemfungia maisha kutojihusisha na soka Mbasha Matutu.

Matutu ambaye ni Msimamizi wa kituo cha Shinyanga na Mjumbe wa Kamati kuu TFF, amefungiwa kwa kosa la kudanganya hesabu ya mapato kati ya mchezo wa Stand United na Simba SC.

Kiongozi huyo kwa sasa amefutwa rasmi wadhifa wake ndani ya Shirikisho hilo akiwa kama Mjumbe wa Kamati Kuu na sasa hatohusika tena na masuala ya soka nchini.

Maamuzi hayo yametolewa na TFF leo kupitia Makao yake yake yaliyopo Ilala, Karume baada ya kuitisha kikao na Waandishi wa Habari.

Whatsapp Button works on Mobile Device only

Start typing and press Enter to search