banner

June 18, 2019

WENGINE WAWILI WASAINI LEO AZAM FC

WENGINE WAWILI WASAINI LEO AZAM FC

UONGOZI wa Azam FC chini ya Ofisa Mtendaji Mkuu, Abdulkarim Amin kwa kushirikiana na benchi la ufundi lililo chini ya Kocha Mkuu, Ettiene Ndayiragaje umewaongezea mkataba wachezaji wake wawili leo ili waendelee kuitumikia timu hiyo msimu ujao.

Nyota hao wawili mikataba yao ilikuwa inamalizika ni pamoja na mlinda mlango Benedict Haule na kiungo Braison Raphael wote wameongeza kandarasi ya mwaka mmoja leo.


Azam FC wanatarajia kuingia kambini kesho kwa ajili ya maandalizi ya michuano ya Kagame wakiwa wao ni mabingwa watetezi itakayofanyika nchini Rwanda mwezi Julai.



Post a Comment

Whatsapp Button works on Mobile Device only

Start typing and press Enter to search