Taarifa zilizotufikia kutoka jijini Mwanza katika dimba la CCM Kirumba ni hatihati ya mechi ya Alliance dhidi ya Simba kufanyika.
Kuna uwezekano mechi hiyo iaksogezwa mbele kutokana na mvua kubwa ambayo inaendelea kunyesha jijini humo.
Taarifa zinasema hali ya uwanja si nzuri kutokana na maji kujaa kwa wingi ndani ya dimba hilo lililo pembezoni kidogo mwa jiji.
Saleh Jembe itaendelea kukujuza kuhusiana na kila kinachojiri juu ya mechi hii inayosubiriwa kwa hamu na wadau pamoja na mashabiki wa soka hapa nchini.
Post a Comment