banner

April 01, 2020

DITRAM NCHIMBI: NINACHUKUA TAHADHARI YA CORONA NA KULINDA KIPAJI

DITRAM NCHIMBI: NINACHUKUA TAHADHARI YA CORONA NA KULINDA KIPAJI


DITRAM Nchimbi, mshambuliaji wa Yanga amesema kuwa kwa sasa anaendelea na programu aliyopewa na Kocha Mkuu Luc Eymael ili kulinda kipaji chake.

Ligi Kuu Bara imesimama kwa muda ili kupisha maambukizi ya Virusi vya Corona ambavyo vimekuwa janga la dunia kwa sasa.

Mshambuliaji huyo anayeaminika kutumia nguvu nyingi uwanjani kuwasumbua mabeki yupo zake mkoani Songea baada ya ligi kusimama.

Nchimbi mwenye mabao sita ndani ya Ligi Kuu Bara na pasi mbili za mabao amesema kuwa anatambua umuhimu wa kuchukua tahadhari kwa ajili ya kujilinda na Virusi vya Corona pamoja na kuendelea kufuata programu alizopewa na kocha ili kulinda kipaji chake.

 "Nipo vizuri ninaendelea na mazoezi ambayo nimepewa programu na kocha hilo ni muhimu kwani kazi yangu ni mchezaji na ninaendelea na mazoezi," amesema.


Post a Comment

Whatsapp Button works on Mobile Device only

Start typing and press Enter to search