banner

March 26, 2024

SIMBA SC YAREJEA DAR TAYARI KUMVUA TAJI AHLY IJUMAA

SIMBA SC YAREJEA DAR TAYARI KUMVUA TAJI AHLY IJUMAA


KIKOSI cha Simba SC kimerejea leo Jijini Dar es Salaam kutoka visiwani Zanzíbar kwa ajili ya maandalizi ya mwisho kuelekea mchezo wa kwanza wa Robó Fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya mabingwa watetezi, Al Ahly.
Simba iliweka kambi ya wiki moja visiwani Zanzíbar kujiandaa na mechi hiyo itakayofanyika Ijumaa kuanzia Saa 3:00 usiku Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.
Timu hizo zitarudiana Ijumaa ya wiki ijayo, Aprili 5 Uwanja wa Cairo International Jijini Cairo, Misri na mshindi wa jumla atakutana na mshindi wa jumla katí ya TP Mazembe na Petro de Luanda ya Angola katika Nusu Fainali.
Ikumbukwe timu hizo zilikutana katika Robó Fainali ya michuano mipya, African Football League na kutoa sare ya jumla ya 3-3, wakifungana 2-2 Oktoba 20 Dar es Salaam na 1-1 Oktoba 24 Cairo, hivyo Al Ahly kwenda Nusu Fainali kwa faida ya mabao ya ugenini.
GONGA KUTAZAMA PICHA ZAIDI


source http://www.binzubeiry.co.tz/2024/03/simba-sc-yarejea-tayari-kumvua-taji.html

Post a Comment

Whatsapp Button works on Mobile Device only

Start typing and press Enter to search