banner

April 25, 2024

SIMBA QUEENS YAIKANYAGA YANGA PRINCESS 3-1 CHAMAZI

SIMBA QUEENS YAIKANYAGA YANGA PRINCESS 3-1 CHAMAZI


TIMU ya Simba Queens imeendeleza ubabe kwa watani wao, Yanga Princess baada ya kuwachapa mabao 3-1 katika mchezo wa Ligi Kuu ya Wanawake Tanzania Bara leo Uwanja wa Azam Complex, Chamazi Jijini Dar es Salaam.
Mabao ya Simba Queens leo yamefungwa na kiungo Aisha Juma Mnunka mawili dakika ya 49 na 90’+2 na mshambuliaji Mkenya, Jentrix Shikangwa Milimu dakika ya 66, wakati bao pekee la Yanga Princess limefungwa na kiungo Mmarekani, Kaeda Wilson dakika ya 90’+5.


source http://www.binzubeiry.co.tz/2024/04/simba-queens-yaikanyaga-yanga-princess.html

Post a Comment

Whatsapp Button works on Mobile Device only

Start typing and press Enter to search