banner

April 24, 2024

ARAJIGA AIFUATA SIMBA SC KOMBE LA MUUNGANO ZANZIBAR

ARAJIGA AIFUATA SIMBA SC KOMBE LA MUUNGANO ZANZIBAR


REFA Ahmed Arajiga wa Manyara ni miongoni mwa waamuzi watatu wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara walioteuliwa kuchezesha Kombe la Muungnao, michuano inayotarajiwa kuanza leo usiku Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzíbar.
Wengine kutoka Bara ni Frank John Komba na Amina Samuel Kyando wakati wa Ligi Kuu ya PBZ Zanzíbar ni wanne, Al Ahmada Mbwana, Ali Ramadhani Ibada, Nasir Siyah ‘Msomali’ na Mohamed Simba Khamis.
Simba itafungua dimba Kombe la Muungano michuano inayorejea baada ya miaka 20 kwa kumenyana na wenyeji, KVZ katika Nusu Fainali leo kuanzia Saa 2:15 usiku Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzíbar wakati Azam FC kesho Azam FC itaumana na KMKM.
Washindi wa mechi za Nusu Fainali watakutana katika Fainali Aprili 27 hapo hapo Amaan Complex.




source http://www.binzubeiry.co.tz/2024/04/arajiga-aifuata-simba-sc-kombe-la.html

Post a Comment

Whatsapp Button works on Mobile Device only

Start typing and press Enter to search