banner

June 24, 2019

MANCHESTER UNITED WAIPIGA CHINI OFA YA NEYMAR

MANCHESTER UNITED WAIPIGA CHINI OFA YA NEYMAR


MANCHESTER United wameipiga chini ofa ya kubadilishana mchezaji wao Paul Pogba na timu  ya Paris Saint Germain (PSG) kumpata Neymar.

Pogba anaonekana ana mpango wa kusepa Old Trafford msimu huu baada ya kusema kwamba ni muda wake sahihi wa kupata changamoto mpya.

Real Madrid na Juventus wote wameonekana wakipambana kuipata saini yake huku Neymar akifikiria kurejea Barcelona.

Mbrazili huyo ameonyesha nia yake ya kurejea timu yake ya zamani ya Barcelona na imeripotiwa kwamba yupo tayari kuomba msamaha ili kurejea Nou Camp msimu huu.




Post a Comment

Whatsapp Button works on Mobile Device only

Start typing and press Enter to search